‎MGOMBEA UDIWANI CCM KATA YA KILIMANI DODOMA AHIDI KUTATUA KERO YA MAJI TAKA.

 


‎Na Edward Winchislaus.

‎Mgombea udiwani kupitia chama cha mapinduzi CCM,Kata ya Kilimani Jijini Dodoma  Mhe.Musa Mkunda  ameahidi kutatua changamoto ya miundombinu  katika kata hiyo iwapo atapewa ridhaa na  wananchi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.2025.

‎Mkunda ameahidi hayo  Septemba 14.2025 wakati wa ufunguzi wa kampeni zake  kwenye kata hiyo ambapo amebainisha kuwa changamoto kubwa inayo wakumba wananchi wa  eneo  hilo  ni pamoja na uwepo wa miundombinu mibovu ya maji taka huku akiahidi kuwa akipata ridhaa ya kuwa diwani ataitatua. 

‎"Mheshimiwa Chinyere hadhara hii yote imeahidi kukupa kura namimi nikiamini unaenda kuwa mbunge wa Dodoma mjini,sisi kata ya kilimani tunachangamoto kubwa ya miundombinu naomba hili mimi na wewe twende nalo kwa miguu miwili ili tuweze kulitatua likiwemo suala la maji taka,"amesema.


‎Aidha mgombea udiwani huyo ametumia jukwaa hilo kumnadi na kumuombea kura mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi CCM  Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan.



‎Kwa upande wake mgombea ubunge katika jimbo la Dodoma mjini kupitia tiketi ya CCM Mhe.Pascal Chinyere amesema tayari serikali imekwisha anzisha mradi wa kujenga bomba kubwa katika eneo la swaswa ili kusukuma maji taka yote yanayo wakumba wakazi wa kata ya kilimani.

‎Pia amesema iwapo watawapa ridhaa ya kuongoza jimbo hilo wataiomba serikali kuwapatia eneo la kujenga  kituo cha Afya katika kata hiyo ili kuwasaidia wananchi wa kata hiyo wanaotembea umbali mrefu kufuata huduma za Afya.


Post a Comment

Previous Post Next Post