DODOMA
UONGOZI wa soko la sabasaba Jijini Dodoma umeanza kutekeleza maagizo ya mwenyekiti wa CCM mkoa Dodoma kwa kuanza kutengeneza njia zilizomo ndani ya soko hilo kwa kutumia kokoto na saraju ili kukabiliana na tatizo la tope nyakati za mvua pamoja na kuepuka magonjwa ya mlipuko kwa wateja wanaofika sokoni hapo
Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa soko hilo Nyamsuka Nyamsuka amesema kuwa hatua hiyo ni kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa Dodoma Adam Kimbisa pamoja Serikali ya Jiji la Dodoma ambayo lengo lake ni kuweka miundombinu bora ndani ya soko ili wafanyabiashara waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.
Nyamsuka ameeleza kuwa ujenzi huo wa njia za ndani ya soko umeanza kwa kudhibiti maeneo yote ambayo yanakuwa kero nyakati za mvua kwa kuwa na tope na madimbwi ya maji ambapo wanaamini shughuli hiyo itakapokamilika adha hiyo haitaweza kujitokeza.
Kwa upande wake mjumbe wa soko hilo Adam Abdalla kombo amesema kuwa ujenzi huo unagharamiwa na wafanyabiashara wenyewe wa soko la sabasaba ambapo kila mwenye banda amechangia shilingi elfu hamsini.




Post a Comment