Mkuu wa wilaya ya Chemba mkoani Dodoma Gerald Mongela amezitaka kamati zinazoshughulikia utoaji huduma ya maji katika ngazi ya jamii wilayani humo kutambua kuwa serikali imewekeza fedha nyingi ili kuhakikisha mwananchi anapata huduma ya maji hivyo visimamie kuhakikisha nia hiyo inafikiwa.
amesema hayo akifungua mkutano wa nusu mwaka wa wadau wa maji wilayani humo wa uwasilishaji na kujadili taarifa ya upatikanaji maji katika wilaya ya hiyo.
Meneja Ruwasa wilaya ya Chemba Mhandisi Robert Mganga ameitaja hali ya upatikanaji maji katika wilaya ya chemba
Kwa upande wake Omary hassan mwenyekiti wa kamati ya utoaji huduma ya maji kata ya Mondo wilayani chemba akitoa wito kwa viongozi wa vijiji kutoingilia utendaji wa vyombo hivyo.
Aidha kamati hizo zinazosimamia utolewaji huduma ya maji wilayani humo zimetakiwa kutimiza wajibu wao kwa weledi ili viweze kujihudumia na kujiendesha vyenyewe.

Post a Comment