Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ametoa rai kwa wakuu wa mikoa kuifanya ajenda ya usafi wa mazingira kuwa
ya kudumu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu
wa Rais Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa
Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya
Uongozi ya Mwalimu Nyerere – Kibaha Mkoa wa Pwani tarehe 26 Agosti, 2023.
Ametoa wito huo tarehe 26 Agosti, 2023 wakati akizungumza wakati wa Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha mkoani Pwani.
Aidha, Waziri Jafo aliwataka wakuu wa mikoa hao kusimamia suala la upangaji wa miji katika maeneo yao ili uwekezaji usikwame kutokana na changamoto za kimazingira.
Alisema kuwa bila kupanga miji vizuri uwekezaji unakuwa ni changamoto kubwa kwani itawalazima wawekezaji kusubiri kupata Cheti cha Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA) kabla ya kuanza hatua ya ujenzi wa miradi.
Post a Comment